Judegment Day At The High Court London

Judegment Day At The High Court London
Mengi v Hermitage: Libel Claim Successfully Defended

Sunday 17 February 2013

Kikwete sanctions corruption of the Mengi family allowing the theft of Silverdale Farm.

 

http://shaabanmpalule.blogspot.co.uk/2013/01/mali-za-umma-zinateketea-katika.html

MALI ZA UMMA ZINATEKETEA KATIKA MASHAMBA YA SILVERDALE NA MBONO-MOSHI KILIMANJARO

 

 

Kiwanda ambacho mbao za Vyama Vya Ushirika wa Uswaa/Mamba, Shari na Kyeeri Zimehifadhiwa, baada ya kukamatwa katika Mashamba ya Silverdale na mbono, Kisha Mahakama kuhamuru zihifadhiwe mahali hapa.

Mbao ambazo zimehifadhiwa katika ghara ya Imara Daima, za wanaushirika wa vyama vya Uswaa/Mamba, Sheri na Kyeeri, zilizotolewa katika Mashamba ya Silverdale na Mbono

Mbao ambazo zimehifadhiwa katika ghara ya Imara Daima, za wanaushirika wa vyama vya Uswaa/Mamba, Sheri na Kyeeri, zilizotolewa katika Mashamba ya Silverdale na Mbono

Kutokana na Mashamba ya Silverdale na mbono kutokuwa na shughuli baada ya mahakama kusitisha, wakazi wa maeneo ya Jirani wamejitokeza kukata kuni kwa ajili ya Matumizi yao Binafsi

Mbao ambazo zimehifadhiwa katika Stoo zilizoko katika Mashamba ya Silverdale na Mbono, ambazo zimeanza kuharibika baa ya kukaa muda mrefu

Kutokana na Mashamba ya Silverdale na mbono kutokuwa na shughuli baada ya mahakama kusitisha, wakazi wa maeneo ya Jirani wamejitokeza kukata kuni kwa ajili ya Matumizi yao Binafs

Mkazi wa Jirani na Mashamba ya Silverdale akitoka kupata kuni katika Mashamba hayo

Mbao ambazo zimehifadhiwa katika Stoo zilizoko katika Mashamba ya Silverdale na Mbono, ambazo zimeanza kuharibika baa ya kukaa muda mrefu

Mkazi wa Uswaa/Mamba, akikata majani katika Mashamba ya Silverdale na Mbono

Wenye viti wa Ushirika wa Uswaa/Mamba, Shari na Kyeeri wakijadili jambo baada ya kutembelea Mashamba ya Silverdale na mbono wakati wa Ukaguzi

Wenye viti wa Ushirika wa Uswaa/Mamba, Shari na Kyeeri wakijadili jambo baada ya kutembelea Mashamba ya Silverdale na mbono wakati wa Ukaguzi, katika jengo la Ofisi lililo katika Mashamba hayo

Sehemu ya Mashamba ya Silverdale na mbono

Sehemu ya Mashamba ya Silverdale na mbono

Wenyeviti wa Ushirika wa Vyama vya Uswaa/Mamba, Shari na Kyeeri wakiwa katika kutathmini uharibifu wa Mbao zinazoendelea kuharibika katika Stoo za majengo yaliyoko katika Mashamba ya Silverdale na Mbono

Wenyeviti wa Ushirika wa Vyama vya Uswaa/Mamba, Shari na Kyeeri wakiwa katika kutathmini uharibifu wa Mbao zinazoendelea kuharibika katika Stoo za majengo yaliyoko katika Mashamba ya Silverdale na Mbono

Wenyeviti wa Ushirika wa Vyama vya Uswaa/Mamba, Shari na Kyeeri wakiwa katika kutathmini uharibifu wa Mbao zinazoendelea kuharibika katika Stoo za majengo yaliyoko katika Mashamba ya Silverdale na Mbono

Wenyeviti wa Ushirika wa Vyama vya Uswaa/Mamba, Shari na Kyeeri wakiwa katika kutathmini uharibifu wa Mbao zinazoendelea kuharibika katika Stoo za majengo yaliyoko katika Mashamba ya Silverdale na Mbono

Wenyeviti wa Ushirika wa Vyama vya Uswaa/Mamba, Shari na Kyeeri wakiwa katika kutathmini uharibifu wa Mashine zinazoendelea kuharibika katika Stoo za majengo yaliyoko katika Mashamba ya Silverdale na Mbono

Hapa wanafungua Milango ambayo ilikuwa aijafunguliwa kwa muda mrefu

Walinzi wa Mashamba ya Silverdale na Mbono, wakifungua Maghara ambayo yamehifadhi Mbao.

Na: Shaaban Mpalule(Moshi)

Wakazi wa Mji wa Hai na Ushirika wa Vyama vya Uswaa/Mamba, Shari na Kyeeri, wameitaka Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Moshi kumaliza Mzozo wa Mashamba uliopo katika Mahakama Moshi Mjini (criminal case no.474/2011, inayowahusu watuhumiwa Dennis Swai na Wenzake wanne katika mashtaka ya kutotii amri halali ya Mahakama iliyoagiza mtu yeyote asifanye shughuli katika mashamba ya Silverdale na mbono.

Wakizungumza katika Mashamba hayo wenyeviti wa vyama vya Ushirika wa Uswaa/Mamba, Shari na Kyeeri, wameiomba mahakama kuangalia kiundani kuhusu kesi hiyo ambayo ilifunguliwa na Benjamini Mengi, ambaye awali alipewa dhamana ya kuwa mwekezaji kabla ya yeye kuliwekeza kwa Waingereza Bw. David Stewart Middleton na mke wake Sara Stewart .

aidha mashamba hayo ambayo yalimilikishwa Vyama vya Ushirika vitatu; yaani Uswaa/Mamba, Shari na Kyeeeri wakati serikali ya Muungano ya Tanzania ilipotaifisha mashamba yaliyokuwa yanamilikiwa na wakulima Wageni Mkoani Kilimanjaro mwaka 1973 na 1974.
Shabaha ya Serikali kumilisha vyama vya ushirika mashamba haya ilikuwa mapato yake yawezeshe wanavijiji husika kusukuma mbele maendeleo yao.

Lakini zaidi ya Miaka 25 tangu mashamba haya yalipokuwa chini ya uongozi wa bodi za vyama vya ushirika hayakuzaa matunda yaliyotazamiwa, Kwa sababu hiyo wakati wa awamu ya tatu ya utawala chini ya uongozi wa Rais Benjamini William Mkapa, Serikali ilishauri vyama vya ushirika kutafuta wawekezaji.

Mnamo tarehe 3 Septemba 1998 washiriki wa vyama vya Uswaa/Mamba, Shari na Kyeeri walifanya mkutano wao wa pamoja uliokaa katika chama cha ushirika Uswaa/Mamba kuwajadili wawekezaji waliokuwa wameomba kuwekeza katika mashamba ya Silverdale na Mbono

Baada ya mazungumzo ya kina wanachama kwa kauli moja waliamua kuwa Fiona Tanzania Ltd ambao wamiliki wake ni Bw. Benjamini A. Mengi na mke wake Millie B. Mengi wapewe kukodishwa kuwekeza katika mashamba hayo kwa vipindi vya miaka mitano mitano.

Kwa mapatano kwamba kila baada ya miaka mitano ,wanachama wa vyama hivi vitatu watakaa na kutathmini maendeleo ya shamba na wakiridhika wanaweza kumruhusu kuendelea kwa kipindi kingine cha miaka mitano.

Mashamba hayo kwa pamoja yana ekari 993 kama ilivyoorodheshwa,

Plot nambari 1 ya hati 9640 ekari 52.4 weruweru, Plot nambari 2 ya hati 9527 ekari 39.4 Weruweru, Plot nambari 3 ya hati 9570 ekari 25.4 Weruweru, Plot nambari 5 ya hati 9377 ekari 28.4 Weruni, Shamba namba 2450 ya hati 11540 ekari 50.0 Weruni, Shamba nambari 9640 ekari 30.5 jumla yake inakuwa 993.1.

Mkataba kati ya vyama hivi vitatu na kampuni ya Fiona Tanzania Ltd uliwekwa sahihi tarehe q januari 1999.Kati ya mambo mengine mkataba uliwataka wakodishiwa wafanye mambo yafuatayo; kulipa kodi ya kila mwaka shilingi 17,500,000 kila ifikapo tarehe 31 Agosti kwa miaka mitano ya kwanza, Kufufua Mibuni iliyopo shambani na kuongeza miche mipya kutoka eneo la ekari 131 za sasa kufikia ekari 300 katika kipindi cha miaka 10 ya kwanza, Kukarabati majengo yote yaliyokuwapo na kuyaweka katika hali nzuri wakati wote, kukarabati majengo yote yaliyopo na mitambo yote inayohusiana na uzalishaji wa kahawa, kutokata miti yoyote iwe kwa matumizi ya mbao,nguzo au kuni bila kibali cha mwenye shamba.

Mnamo tarehe 21 mei 2004 Kampuni ya Fiona Tanzania Ltd, iliingia mkataba na David Stewart Middleton, hapo mbeleni Bw. David S. Middleton alikuwa ameajiriwa na Bw. Benjamini Mengi kama Consultant Agronomist chini ya Kampuni ya Alpha Tobacco T. Ltd ambayo ilikuwa chini ya Bw. B.A. Mengi ambayo kusudi lake ilikuwa kuendesha mashamba ya tumbaku.

Katika mkataba huo mpya kati ya Kampuni ya M/S Fiona T. Ltd na David Stewart Middleton mashamba ambayo yalikuwa yamekodishwa na kampuni ya M/S Fiona T. Ltd kutoka kwenye vyama vitatu vya Ushirika, yaani; Uswaa/Mamba, Shari na Kyeeri, hawa wawili waliamua kuyaingiza katika kampuni yao mpya kwa jina la Silverdale T. Ltd; wao wenyewe wakiwa ndiyo wakurugenzi. Bw. David S. Stewart Middleton akiwa na hisa asilimia 70 na Bw. B.A. Mengi asilimia 30. Kamapuni hii Mpya Silverdale T. Ltd ilikuwa iendeshe shughuli zote ambazo M/S Fiona T. Ltd ilikuwa ikizifanya kwenye mashamba ya Silverdale na Mbono. Mkataba huo ulitayarishwa kwa mapatano kwamba Bw. David Stewart Middleton angemlipa Bw.B.A. Mengi kiasi cha USA $ 112,000 yaani fedha za kitanzania kwa thamani ya leo ya Shs. 1,150 ni sawa na shilingi 128,800,000/=.

Kwa kuwa wadau wa mashamba hayo yaani washirika wa vyama hivyo vya Ushirika vitatu-Uswaa/Mamba, Shari na Kyeeri ilipasa wajulishwe nia ya mabadiliko hayo mapya na waweze kuridhia, jambo ambalo halikufanyika, ila inaonekana kuwa marekebisho ya mkataba huo yaliwekwa sahihi na wenyeviti wa vyama hivyo vitatu bila mihuri ya vyama husika.

Hapo ndipo penye utata wa aina mbili ambao ni mkubwa sana; kwanza, kampuni ya Fiona T. Ltd ambayo ilipaswa kutaarifu vyama husika nia yake ya kutaka kufanya marekebisho ya mkataba wa kwanza hawakufanya hivyo; pili, wenyeviti walioweka sahihi kuwakilisha vyama husika hawakuweka mihuri ya vyama vyao kuhalalisha ridhaa yao.Pamoja na tata mbili zilizotajwa hapo juu, upo utata mwingine ambao ni wa msingi kabisa. Afisa wa vyama vya Ushirika Wilaya ya Hai alipopata habari kuhusu kusudio hilo la kutaka kufanya marekebisho ya mkataba wa kukodisha mashamba hayo aliweza kuandika barua kwa wenye viti wa vyama hivyo kuwataka kusitisha kuweka sahihi mkataba huo mpya hadi wanachama wa vyama vyote vitatu watakapojulishwa kwenye mkutano wao wa pamoja . Barua hiyo ya tarhe 11 mei,2004 yenye kumbukumbu Na. LY/C.40/32/2 haikuwekwa maanani na wenyeviti hao. Hapa inaonekana kwamba ulikuwapo ujanja na hila ambayo haiwezi kukanushwa kwa urahisi. Mwekezaji Fiona T. Ltd na pia wenye viti wa vyama vitatu vya Ushirika wanapaswa wajieleze kwa nini walipuuza barua halali ya Afisa Ushirika wa Wilaya.

3. Mkutano wa wanachama wa vyama vitatu-uswaa/mamba,shari na kyeri.

Kutokana na fununu zilizosikika na baadhi ya washirika wa vyama vya ushirika kuwa ulikuwepo ugomvi kati ya Bw.B.A Mengi na mshirika wake Bw.David Stewart Middleton kuhusu mashamba ya Silverdale/Mbono walitaka uongozi wa vyama vitatu viite mkutano ili wanachama waelezwe kilichokuwa kinaendelea katika mashamba hayo.

Hatimaye mkutano uliitwa;wanachama wa vyama vyote vitatu yaani Uswaa/Mamba,Shari na Kyeeri wakakutana katika uwanja wa soko la Bwani karibu na chama cha ushirika shari tarehe 17.1.2006

Mahudhurio ya kikao:

1. Wajumbe wanachama 300

2. Wajumbe wa Halmashauri ya vyama vitatu

3. Wajumbe wa Halmashauri ya mashamba Silverdale na Mbono

4. Afisa ushirika Hai Bw.R.A Masamu,

5. Msaidizi wa Afisa Ushirika Hai Bw.Fura Uroki

6. Bw. Menjamini A Mengi –Mwekezaji (Fiona T Ltd)

Wajumbe wa mkutano walielezwa historian na malengo ya uwekezaji katika mashamba ya Silverdale na Mbono.Pia wakajulishwa kwamba miaka mitatu ya kwanza hapakuwepo matatizo kati ya mwekezaji na wamiliki wa shamba.Kwamba mwekezaji alilipa kodi yake kwa wakati ila bodi ya mashamba haikuita mkutano wa wanachama wa vyama vyote vitatu kwa pamoja kwa kipindi cha miaka saba;yaani 1999-2005 kama ilivyotazamiwa kuwaeleza maendeleo ya mashamba yaliyokodishwa na mwekezaji.Vile vile hawakupewa tafsiri ya Kiswahili ya mkataba kama walivyokuwa wamedai hapo mbeleni waliposomewe mkataba wa kwanza kwa kuwa wengi wa wanachama hawakujua kiingereza.

Baada ya mazungumzo ya muda mrefu,maswali na majibu kutoka kwa wajumbe wa halmashauri ya zamani na mpya,na pia mwekezaji Bw.Benjamen A.Mengi mkutano mkuu uliazimia yafuatayo:-

a) Kwamba Halmashauri ya zamani ya mashamba ivunjwe mara moja.

b) Kwamba halmashauri ya vyama vitatu-Uswaa/Mamba,Shari na Kyeeri ichukue wajibu wake mara moja.

c) Kwamba mkutano mkuu hautabui Bw.David Stewart Middleton ila unatambua mwekezaji ambaye ndiye aliyeandika mkataba nao,yaani Fiona Tanzania Limited.

d) Kwamba Halmashauri za vyama vitatu-Uswaa/mamba,Shari na Kyeeri siteue kamati ndogo miongoni mwake ambayo ndiyo itakayochukua wajibu zote badala ya Bodi iliyovunjwa kwa niaba yake.

e) Kwamba kamati mpya izuru mashamba hayo mara moja na kuona hali ilivyo.

f) Kwamba kamati hiyo iangalie mkataba uliopo kama kuna dosari ichukue hatua za kuurekebisha.

itaendelea kesho

No comments: